Mtendaji
Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Prof. Dos
Santos Silayo amewaasa wananchi kutonunua maeneo ya ardhi ndani ya Hifadhi ya Msitu wa Kazimzumbwi yanayouzwa
na wavamizi.
Akizungumza
mwanzoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, Prof. Silayo alisema Serikali
haijabadili matumizi ya Hifadhi ya Msitu wa Kazimzumbwi ulioko Kisarawe mkoani
Pwani, na kwamba eneo hilo lisikaliwe na raia yeyote au kutumika
kwa namna nyingine yoyote kama ilivyotanganzwa na tangazo la Serikali Na. 306
lililochapishwa 24/9/54 AN 4/67/20.
Aliyazungumza
hayo mara baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Mkurugenzi wa Usimamizi Rasilimali za Misitu, Bw. Zawadi Mbwambo kuwa kuna watu wamevamia
Hifadhi ya Msitu wa Kazimzumbwi na kuanzisha makazi na wengine wanafanya
shughuli nyingine za kibinadamu ikiwemo kuuza viwanja.
Alisema kinachofanywa na wavamizi hao
ni kinyume na sheria na Serikali haitawavumilia wale wote waliovamia na
kuanzisha makazi ndani ya maeneo ya hifadhi ya msitu na hivyo kuwataka waondoke haraka.
“Kuna
watu wanauziwa viwanja kwa bei rahisi katika Hifadhi ya Msitu wa Kazimzumbwi iliyoko
karibu kabisa na makazi ya watu nawaasa wananchi msikubali kutapeliwa! Ukinunua
nawe unakuwa mvamizi na TFS na Serikali kwa ujumla haitajali kuwa umepewa hati
miliki au la, hilo ni eneo la msitu wa hifadhi na shughuli zozote za kibinadamu
haziruhusiwi, utalazimika kuondoka tu.”
Msitu
wa Hifadhi wa Kazimzumbi wenye eneo la ardhi lipatalo hekta 12,015,
lililopo Wilaya ya Kisarawe Kusini na Kusini – Magharibi ya Boma la Kisarawe,
Magharibi ya barabara ya Pugu – Chanika, Kaskazini ya njia ya Chanika – Masaki
na Kusini ya barabara ya Dar es Salaam – Morogoro kwa kiasi kikubwa hutumika
kuvuta hewa chafu inayotokana na viwanda na mlundikano wa magari ya jiji la Dar
es Salaam na mikoa ya karibu yake.
Chini ni tangazo la Selikali la Mwaka
1954 likiutangaza Msitu wa Kazimzumbwi kuwa ni Msitu wa Hifadhi:
TANGANYIKA GAZETTE,
Jal. XXXV Na. 54 tarehe 24 Septemba, 1954
TANGAZO LA SERIKALI
NA. 306 LILILOCHAPISHWA 24/9/54 AN 4/67/20
SHERIA YA
MISITU
(KIF. 132)
TANGAZO
(Chini ya sehemu ya 4 ya Sheria ya
Misitu)
TANGAZO LA HIFADHI YA MSITU WA
KAZIMZUMBWI
E.F. TWINING,
Gavana.
KWA KUWA MIMI, EDWARD FRANCIS TWINING,
Gavana na Amiri Jeshi Mkuu wa Tanganyika, nimeridhika kuwa inafaa kulifanya
eneo la ardhi ya umma lililomo ndani ya mipaka iliyoelezwa katika Jedwali
iliyoambatanishwa liwe ni hifadhi ya msitu, na kwamba eneo hilo lisikaliwe na
raia yeyote au kutumika kwa namna nyingine yoyote.
HIVYO BASI, SASA, kwa mamlaka
niliyopewa katika sehemu ya 4 ya Sheria ya Misitu, nalitangaza eneo lililotajwa
kuwa ni hifadhi ya msitu.
JEDWALI
WILAYA YA KISARAWE, JIMBO LA
MASHARIKI
Hifadhi ya Msitu wa Kazimzumbwi – Eneo
lote la ardhi linalofikia karibu ekari 12,015, lililopo Wilaya ya Kisarawe
Kusini na Kusini – Magharibi ya Boma la Kisarawe, Magharibi ya barabara ya
Pugu-Chanika, Kaskazini ya njia ya Chanika – Masaki na Kusini ya barabara ya
Dar es Salaam – Morogoro (Rejea ya Ramani ya Nchi 1:1,000,000 sheet, Kusini B37
(F VI) kama ilivyofafanuliwa katika Mpango wa Idara ya Misitu Na. JL 196
iliyowekwa katika Idara ya Ardhi na Upimaji na Mipaka yake ni kama
ifuatavyo:
Mashariki – Kuanzia boya Na. 1
kwa upande wa Kusini kwenye njia panda ya Barabara ya Dar es Salaam –
Maneromango na njia ya kwenda kwenye kituo cha chini cha pampu ya maji cha
Kisarawe futi 1,150 Kusini kufuata njia hii hadi kwenye boya Na. 2; kutoka hapo
futi 254 kufuata nyuzi 295 hadi kufikia boya Na. 3 kufuata njia ya bomba la
maji kuelekea Kisarawe Bomani; kutoka hapo kwa kulifuata bomba hili kuelekea
Kaskazini – Mashariki kwa kukatiza mstari wa maboya unaovuka Mto Pwani kwa futi
7,136 hadi boya Na. 21. Kutoka kwenye boya Na. 21 kufuata uwelekeo wa Kusini
kwa kukatiza mstari wa maboya kwa futi 8,135 kuvuka Mto Kakurongo na Mto Zumbwi
hadi kwenye boya Na. 35; kutoka hapo kwa kufuata uwelekeo wa Kaskazini –
Mashariki kwa futi 2,085 hadi kwenye boya Na. 38; kutoka hapo Kusini –
Magharibi kwa futi 7,735 hadi kwenye boya Na. 49 kwa kupitia Magharibi ya
kijiji cha Nyeburu. Kutoka boya Na. 49 Kuisini – Mashariki kwa futi 3,185 hadi
boya Na. 35, kutoka hapo Kaskazini – Magharibi kwa futi 1,972 hadi boya Na. 55
na kutoka hapo Kusini – Mashariki kwa futi 1,438 hadi boya Na. 56. Kutoka boya
Na. 56 Kusini-Magharibi kwa futi 9,021 kuvuka Mto Mzinga na Mto Vikongero hadi
boya Na. 64, kutoka hapo Kusini – Mashariki kwa futi 5,044 kuvuka Mto Bulampuka
na Mto Nzasa hadi boya Na. 70; kutoka hapo Kusini-Magharibi kwa futi 7,667 hadi
boya Na. 79 karibu na kijiji cha Nzasa na futi 214 Kaskazini ya njia ya
Chanika-Masaki.
Kusini:- Kutoka boya Na. 79
karibu na kijiji cha Nzasa kwa mkato kupitia mstari wa maboya kufuata uwelekeo
wa magharibi kwa futi 10,104 kuvuka Mto Mnyonde hadi boya Na. 96 kwenye mlima
Mnyundo karibu na kijiji cha Maguruwe.
Magharibi:- Kutoka boya Na. 96
kwenye mlima Mnyundo kwa mkato kupitia mstari wa maboya kufuata uwelekeo wa
Kaskazini kwa futi 20,704 kuvuka mto Mwangulinga hadi baya Na. 136 Kusini ya
kijiji cha Kazimzumbwi, kutoka hapo bado kwa kufuata uwelekeo huo huo wa
Kaskazini kwa futi 4,564 kufuata njia hadi kwenye boya Na. 137; kutoka hapo kwa
mkato na kufuata mstari wa maboya kwa futi 1,938 hadi kwenye boya N. 141.
Kutoka kwenye boya Na. 141 kufuata uwelekeo wa Mashariki kwa futi 1,942 kufuata
njia hadi boya Na. 142; kutoka hapo kwa mkato na kufuata mstari wa maboya
Kaskazini Mashariki kwa futi 11,072 kuvuka Mto Zumbwi hadi kwenye boya Na. 157
lililopo zizi la Mvule kwa upande wa Kusini wa Barabara ya Dar es Salaam –
Morogoro.
Kaskazini:- Kutoka kwenye boya
Na. 157 lililopo Zizi la Mvule katika Barabara ya Dar es Salaam – Maneromango
kufuata upande wa Kusini wa barabara Mashariki kwa futi 2,530 hadi boya Na.
158; kutoka kwenye boya Na. 158 kwa mrengo wa kadiri ya nyuzi 105 kwa futi 891
hadi boya Na. 159, kutoka hapo kwa mrengo wa kadiri ya nyuzi 214 kwa futi 2,325
hadi boya Na. 160; kutoka hapo kwa mrengo wa kadiri ya nyuzi 13.50 kwa futi
2,350 hadi boya Na. 162; hivyo kijiji cha Vazama kipo nje ya hifadhi. Kutoka
boya Na. 162 kwa mkato na mstari wa maboya kwa futi 3,576 kwa mwelekeo wa
mashariki hadi boya Na. 166 kwa upande wa mpaka wa Magharibi wa shamba la
mipira E.P.L 899 (Registered Plan E1 230/6535). Kutoka boya Na. 166 kufuata
njia Kaskazini kwa futi 4,276 hadi boya Na. 167 kwa upande wa Kusini ya
Barabara ya Dar es Salaam – Morogoro; kutoka hapo kwa upande wa kusini ya
barabara Mashariki kwa futi 3,265 hadi boya Na. 1, ambapo ilipoanza
hifadhi.
Sehemu zifuatazo siyo sehemu ya hifadhi
ya msitu:
Sehemu ya ardhi iliyokatwa na kuwekwa
maboya ipatayo ekari 170 ijulikanayo kama kijiji cha Obani.
(ii) Shamba la mipira kadiri ya ekari
255 lililosajiliwa chini ya mpango Na. E1 250/6535.
Viwanja vinavyouzwa ndondwe huko chanika vip ni vya misitu au?
ReplyDelete